1 2 3 4 5 6 7 8 9 10

1

IMAGE imgs/Swahili01.gif

Watu mia moja na nne, waume, wanawake na watoto walipanda ndege aina ya MI 185 tarehe19 Desemba 1997 kutoka Jakarta.

Wakati ndege ilipokuwa ikinapaa kuelekea Singapore, hakuna hata mmoja wao aliyeweza kujua kuwa hawatafika mwisho wa safari yao. Ndege yao Boeing 737 aina ya Jeti ghafla karibu na Palembong ilipiga mbizi na kupasuka vipande vipande karibu na Sungei Musi, na kuua abiria wote pamoja na wafanyikazi wote wa ndege hiyo.

Watu wote duniani wanapata majanga makubwa ya vifo, matetemeko ya ardhi, vimbunga, ajali mbali mbali. Hayo ni mifano ya majanga yanayo kuja ghafla bila kutegemea, hivyo watu wanakuwa hawana uwezo wa kudhibiti vifo vya namna hiyo.

Watu wengine wanakufa kutokana na magonjwa yasiyotibika. Kila mmoja wetu anajaribu kujitayarisha kwa ajili ya kifo, lakini kifo siku zote hakitabiriki na hakidhibitiwi.

Baadhi ya watu wanajaribu kuishi maisha marefu kwa kutovuta sigara na kufanya mazoezi ya viungo, kula vyakula bora, pamoja na kunywa vidonge vyenye kuongeza afya (vitamini). Pamoja na hayo, hatuwezi kukataa ukweli kuwa siku moja tutakufa.

Watu wengine hawafikirii kuhusu kifo, wakati wanapokuwa hawakabiliwi na matatizo, wakati wanapokuwa na uwezo wa kuwa na chakula na fedha, wakati hakuna matatizo ya kifamilia na wanapokuwa na nafasi/ cheo katika jamii, kifo kinakuwa mbali na mawazo yao. Lakini kifo hakifiki kwa watu wazeena wenye shida tu, pia watu wenye akili na vijana wanaweza kufa bila taarifa. Kifo kinaleta usawa kwa wote tokia tabaka kwa juu hadi tabaka ya chini.

Mungu, ana madaraka ya kutuweka mbinguni na kutuhukumu jehanamu kulingana na hukumu yake. Jina lake Ar Rahmani Rahim [yeye Masiha na mkamilifu] hivyo anatuonya tujihadhari na kujitayarisha wakati wote kwa kifo na kiama . Kila mtu atakufa siku mmojana badaye kuhukumiwa siku ya hukumu, wakati kila moja atahukumiwa kutokana na matendo yake aliofanya wakati wa maisha yake duniani

Hivyo Mungu anatutaka, tuwe tayari muda wotekuanzia sasa. Aliye tayari wakati wowote ni yule anaye tembeya katika njia iliyo nyoofu katika amani ambayo Mungu pekee ndiye anatoa.